Album Cover Kiberiti

Kiberiti

Fid Q

4

(Lu-Lu-Lufa)

Haueleweki hata uki-shine kwa punchlines on FacebookHaiwi-fine ka′ Rayvan, we' fake tu

Sikuoni B.E.T au MTV wak-play tunes

Miaka nenda we′ msanii, MC una play tu

Makida, we' sio king kama Kiba

Sio yao ming kwenye ring

Mistari mingi zaidi ya zebra? (Zaidi ya zebra!)

Unazingua nigga, haujajijua nigga

Umeanguka pua, bishoo hauwezi kuwa Jigga

Rent mwezi ujao na haujalipa school fees

Ya mwanao, unaumiza kichwa ewe Q-Fid

'Til now hauioni future, we′ stupid

Haujapiga bao na kutwa unawaza groupies?

Pengine ni nuksi umejiletea au chuki umejijengea

Haukumbuki ulipotokea bro (bro)

Wabaya mauzushi, wanayachochea haushtuki ushapotea

Wakushi wanakutetea bro

Unakosea bro, ni kweli hauna spear bro

Ku-play fair, ikuwachezea ikatokea droo

Sikutegemea bro, hatuwezi hataku′onea bro

Tushajionea ulivyo mlevi, ukaikosea show

Kiberiti, ninakuona unavyoniwashia moto mie (aye)

Kiberiti, ninakuona unavyoniwashia moto mie (aye)

Ayi, ma-mama, kiberiti

Ayi, ma-mama

Nikiwa alone in my room, sometimes I stare at the door

And in the back of my mind, naziita hisia hebu njoo

Zinaingia zinaniambia hii dunia ni soo

Haiko sweet kama dove, I see, I need love

Tazizo lako hautaki kuuza maneno

Legeza ka' wenzako acha kutukuza misemo (kutukuza misemo)

Sheria ni yako ila isiuache msumeno

Ukijikuna tako, usikate kucha kwa meno

Ongea usikike au kaa kimya usidharaulike

Au utupishe na jina lisahaulike

Tulazimike kuzima ili itulipe

Gwajima tumuite aje kukupima heshima ya Bashite

Nje ya town, show huwa zina cloud ya kiwaki

Kaza crown ibaki, ukikaza sana hawataki

Tunajua una uwezo wa juu na kismati

Na haujawahi kupigwa bu! Basi unajiona Tupac

Kabla ya rotten brothers ulikua na chepe

Two nature boys ndiko ulikoanza makeke

Mwaka huu, mwaka we mwaka

Ikakuweka juu ikawa Q hakuna asiyemtaka, well

Lini uta-retire urudi kuuza mtumba lango?

Una roho mbaya, hadi leo haujamkumbuka Rado

We′ sio kichwa, we' unaweza fichwa

Ikichorwa hip hop, siioni sura yako picha

Kiberiti, ninakuona unavyoniwashia moto mie (aye)

Kiberiti, ninakuona unavyoniwashia moto mie (aye)

Ayi, ma-mama, kiberiti

Ayi, ma-mama

Fid Q nikuulize, hivi siri yako nini kuishi kwenye game muda mrefu, eh?

Kwanza unajua, mi′ huwa sichukulii vitu personal

Ukiniponda sichukulii personal, ukinisifia sichukulii personal

Ni'chojifunza ni kwamba usichukulie kila kitu personal

Na zaidi, ufunze ubongo wako kung′amua jema kwenye situation yoyote ile

Na hivi ndio vitu ambavyo Don Miguel kwenye kitabu chake cha The Four Agreements ameviongelea

Kwa mfano, nikikutana na wewe sokoni au kokote na nikakuambia, "Wewe ni mjinga"

Wakati hata sikujui, na siku hiyo hiyo ndio mara ya kwanza tumeonana

Anaekua amevurunda hapo sio wewe ni mimi

So kwa wewe kuchukulia personal na ku-react

Ni sawa kuwa umekubaliana kihisia na jina hilo la mjinga

Na huenda ukanifanya nijione mimi ni muoteaji mzuri

Kuchukuria kitu personal ni kukubaliana moja kwa moja na kilichosemwa

Na kama kweli umekubaliana inamaana kimekuingia

Na kinapokuingia husambaza sumu ambayo huziua zile fikra chanya

Ulizokuwa nazo na kufanya usichukue maamuzi sahihi

Kila mtu anafanyanya vitu kwa ajili yake na kwa faida anazozijua yeye mwenyewe

Ni mara chache sana wewe kuzing'amua hizo faida binafsi za watu

Wengine utaona ni kwa ajili ya attention

Wengine ni kwa sababu inawaingizia kipato

Wengine iyo kitu huwaacha tu na furaha ya moyo

Na vitu kadhaa wa kadha

Kila mtu ana ndoto zake na pia hupendelea kufanya vile akili yake inamtuma

Na pengine dunia tunayoishi sisi sio dunia wanayoishi wao

Hivyo tunavyochukulia vitu personal ni sawa na kuwa-

Kuwaaminisha ya kwamba tupo kama wanavyotufikikiria

Na tunaota kuwa na utulivu kama walionao wakati sio kweli

Na hata tusi liwe la nguoni kiasi gani

Ni vyema ukajua na kuamini ya kwamba halikuhusu

Kumbuka limjaalo mtu ndilo limtokalo

Wengine wameathiliwa na malezi waliopitia pamoja na makuzi kwa ujumla

So, hata mtu akiniambia we, yani

Kwa mfano mtu akikwambia, "We Saida ni mshamba kuliko wasanii wote Tz"

Ni vyema ukamsamehe tu!

He! Lakini kumbuka kumsamehe mtu inamaana alikukwaza

Uka-mind ndio maana ili usimfugie chuki na hasira

Ndio maana inabidi umsamehe

Na kumkasirikia inamaana uliruhusu ile sumu ikuingie

Kwa hiyo kwenye hili mtu akikwambia, "Wewe ni mshamba kuliko wasanii wote"

Tunashauriwa kumuacha kama alivyo tu

Kwa sababu hizo ni hisia, imani na maoni yake yeye binafsi

Na dawa pekee ya kuituliza iyo sumu

Ni kuwapotezea tu ili waendelee kupambana na hali zao

Watu wengi huwa wanashindwa kumjaji mtu kama alivyo

Kutokana na vitu alivyonavyo

Cha ajabu mentality hii imetupelekea sisi kuacha au kusahau kabisa

Kuchukulia vitu kama vilivyo na kuanza kuvichukulia kama tulivyo

Kiberiti, ninakuona unavyoniwashia moto mie (aye)

Kiberiti, ninakuona unavyoniwashia moto mie (aye)

Ayi, ma-mama, kiberiti

Ayi-yi, ma-mama

Ninashangaa

Kumbe wanadamu ndivyo walivyo

Kumbe wanadamu ndivyo walivyo

Ayi, ma-mama

Ayi-yi, ma-mama

Ninashangaa

Kumbe wanadamu ndivyo walivyo

Kumbe wanadamu ndivyo walivyo

Lagu lain oleh Fid Q